IWAPO UMEANZISHA THREAD (UZI) JAMIIFORUMS, NA THREAD YAKO IKATIWA KAPUNI NA MODS. JIBU LAKO LIPO KWENYE BLOGU HII. TUPIA UZI HUO ILI TUUWEKE OPENLY TUPIA KWA EMAIL: jamiiforumsblog@gmail.com

Wengine Wanasemaje?

Sunday, July 29, 2012

SMS KALI ZA MAPENZI

Wakuu wa Jukwaa La Malavedave;

Bila ya shaka wengi mmewahi kutuma au kupokea SMS za Mapenzi kuhusiana na subject mbalimbali katika mapenzi. Hata hivyo kuna zile ambazo zinafurahisha sana na pia kutia raha mara ukisoma. katika hizo chache nilizokutanaza nazo. Naomba, usome, tafakari, cheka, kisha na wewe tuambie ni SMS gani ulizokutana nazo ambazo ukizikumbuka zinakufurahisha?

  • Najiuliza kila leo hivi ni mimi tu kimeo katika dunia hii ya leo maana kila leo nayempata huishia kunipa ahadi kila leo, mpenzi kila siku waniaidi mara nitakupa leo mara kabla ya machweo, hivi ni lini utanipa jibu la uhakika nakunipa mapenzi ya uhakika nipate farijika? Nakupenda mpenzi.

  • Kila siku najiuliza moyoni hivi ni nini nilichokukosea jamani? Mitaani sikuoni, hata njozini pia huonekani hivi kweli upo hapa duniani? Naamini nitapata kusikia toka kwako siku za usoni,nimekumiss nakueleza toka moyoni, zaidi kumbuka haya siyo maisha wanayoishi marafiki duniani!

  • Hakika mtoto umeumbika mithili ya malaika japo mbinguni sijafika lakini nauhakika kwa kila mwanaume aliyeumbika na kukamilika akikuona lazima udenda utamtoka, naomba japo yako dakika nipate kukueleza moyoni yaliyonifika kwani siwezi tena kuficha jinsi navyokupenda, nakupenda amini kwako nimefika!

  • Nakupenda dear, amini moyoni umeniingia ndiyo maana mimba nikaamua kukubebea pasipo kunioa hakika mahaba yako yanifanya nijione malkia katika hii dunia! Nakupenda

  • Ukweli lazima nikwambiye kwa kuwa sina kimbilio nakupenda kijana mwenzio sijui kwanini hutaki kukisikia changu kilio, namwomba Mungu kila kukicha usikiye changu kilio, nakupenda na kama kukueleza hili nakukosea nisamehe kwani si langu kusudio,luv u mwaah.
Je, Ni SMS gani za kufurahisha za mapenzi umewahi kukutana nazo? share with us with a light touch.

Peace and Love.

Respect

mdau

ZITTO: SIJAHONGWA, NI SIASA ZA POSHO NA URAISI

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Mashirika ya Umma ambayo imeunganishwa kwenye tuhuma hizo, Zitto Kabwe, alisema tuhuma hizo anazisikia, lakini anaziona kama siasa za majitaka kwa sababu zinarushwa bila ushahidi wowote.

"Hakuna hata mbunge mmoja aliyesimama kusema nani amehongwa nini. Mimi binafsi sijahongwa na mtu yeyote wala mimi sijamtetea mtu isipokuwa natetea taratibu kufuatwa," alisema.

Zitto alibainisha kuwa anaamini tuhuma hizo zimetokana na hasira za yeye kupinga posho za wabunge na sasa wameona hilo ndilo eneo la kumkomoa.

"Kwa kuwa ‘my conscious is clear’, (dhamira yangu safi) sina mashaka, uzushi, uongo na siasa za majitaka hizi zitaumbuliwa na ukweli. Hata hivyo, kwa kuwa tuhuma hizo zinasemwa juu juu tu, tutataka vyombo vya dola vichunguze na ikithibitika hatua zichukuliwe," alisema na kuongeza:

"Kwangu mimi naona hizi ni siasa za urais na hasira za posho. Wenye kutaka urais wa vyama vyote na wapambe wao, wameungana kunichafulia heshima yangu. Wabunge wenye njaa ya posho, wameungana kunikomoa. Ukweli una tabia ya kutopenda kupuuzwa. Mwalimu Nyerere (Julius) alisema katika andiko lake la 'Tujisahihishe'.”

Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini(Chadema) alishauri pia Spika wa Bunge kutumia Kamati ya Maadili kuchunguza tuhuma hizo kwa kuwa hazipaswi kuachwa zikapita hivihivi.


Source: Mwananchi Jumapili.